Follow by Email

Wednesday, May 9, 2012

Tanzania pledges to pursue Genocide Fugitives


Hon. Bernard K. Membe (MP), Minister for Foreign Affairs and International Cooperation, in talks with Hon. Judge Theodor Meron, President of the International Residual Mechanism for Criminal Tribunals (IRM), today when the Judge paid a courtesy call to the Minister's office in Dar es Salaam.  


Hon. Bernard K. Membe (MP), Minister for Foreign Affairs and International Cooperation in talks with the six member delegation from the International Residual Mechanism for Criminal Tribunals (IRM), that visited him today in his office.  The delegation included Judge Theodor Meron, President of the International Residual Mechanism for Criminal Tribunals (IRM), Hon. Judge John Hocking, Registrar of the IRM and Hon. Hassan Bubacar Jallow, the Prosecutor of the IRM.

Tanzania pledges to pursue Genocide Fugitives
Hon. Judge Theodor Meron, President of the International Residual Mechanism for Criminal Tribunals (IRM), paid courtesy call to Hon. Bernard K. Membe (MP), the Minister for Foreign Affairs and International Cooperation today in his office, following his recent appointment as IRM President.
Hon. Meron was accompanied by Hon. Judge John Hocking, Registrar of the IRM and Hon. Hassan Bubacar Jallow, the Prosecutor of the IRM.
Judge Meron thanked Tanzania for once again accepting to host the International Criminal Tribunal and hoped that Tanzania would sustain the same level of cooperation as it had existed during the lifetime of the International Criminal Tribunal for Rwanda (ICTR).
He also thanked Tanzania for granting land for construction of the purpose-built facility for both the IRM premises and ICTR archives.
The delegation also asked the Government to assist in pursuing nine remained fugitives remained at large within the East and Southern African Regions.
On his part, Hon. Membe thanked the delegation for the visit, and for the interactive exchange regarding IRM.  He also expressed apologies on behalf of the President for not being able to meet the delegation as it was planned.
Hon. Membe informed the delegation that President Jakaya Kikwete expressed readiness to meet the delegation in the near future.
With regard to the issue of land offered to the IRM, the Minister expressed his enthusiasm on the fact the United Nations (UN) has confirmed its desire to take up the offer of the land allocated to the IRM.  
Hon. Membe assured the delegation that the Government will facilitate the logistical requirements towards the construction of the facility.
He also assured the delegation that Tanzania will do all it can to support the IRM in apprehension of the said nine fugitives.   
The IRM was established by the United Nations Security Council (UNSC) Resolution 1966 (2010) to finish the work begun by the ICTR and International Criminal Tribunal for the former Yugoslavia (ICTY). The IRM has two branches corresponding to the two current tribunals.  The Arusha branch is scheduled to start on July 1, 2012 while the Hague branch is scheduled to start on July 1, 2013.   
  



Msimamo wa Tanzania kuhusu Sahara Magharibi




Mhe. Bernard K. Membe (MB), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akitoa msimamo wa Tanzania kuhusu suala la Sahara Magharibi na Morocco, wakati akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam.  
 

Mhe. Bernard K. Membe (MB), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akitoa msimamo wa Tanzania kuhusu suala la Sahara Magharibi na Morocco, wakati akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam.

 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (MB), akijibu maswali mbalimbali yaliyoulizwa na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa Mkutano wa Wizara ya Mambo ya Nje leo jijini Dar es Salaam.  Mwingine pichani ni Bw. Assah Mwambene, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali -Wizarani.
 
 
 
 
Msimamo wa Tanzania kuhusu Sahara Magharibi
 
Tanzania imesema haijabadili msimamo wake katika kuwaunga mkono Watu wa Sahara Magharibi kuhusu haki yao ya kujitawala kutoka mikononi mwa Morocco.

Hayo yalisemwa na Mhe. Bernard K. Membe (Mb), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakati akiongea na Waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari leo jijini Dar es Salaam.

Aidha, Tanzania imeisihi Morocco irudi katika uanachama wa Umoja wa Afrika ili kuweza kuwa na mazungumzo ya pamoja baina yao, wananchi wa Sahara Magharibi na Umoja wa Mataifa kwa lengo la kutafuta suluhu ya kudumu kuhusu mgogoro huo.

“Tatizo hilo limekuwa kidonda ndugu haliwezi kupona kesho, kwa hiyo msimamo wa Tanzania ni huo. Tunataka kuwe na uhuru wa Sahara Magharibi na tunaomba pande zote, pamoja na Umoja wa Mataifa wamalize kwa haraka sana tatizo hili ili kuwe na kura ya maoni ya wananchi wenyewe kuamua ama kujitawala au kuwa sehemu ya Morocco,” alisema Mhe. Membe.

Mhe. Membe aliongeza kuwa, Tanzania itaheshimu maamuzi yoyote ya wananchi wa Sahara Magharibi kwa vile “tunaamini wataamua kujitawala wenyewe na siyo kuwa kama kile Kisiwa cha Mayote nchini Comoro”.  Wananchi wa Kisiwa hicho waliamua kuwa sehemu ya nchi ya Ufaransa, ingawa kipo Afrika.

Kuhusu tatizo la kumpata Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika (AU), Mhe. Membe alisema Tanzania inaungana na Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) kumuunga mkono mgombea kutoka Afrika Kusini kwenye nafasi hiyo Bi. Nkosazana Dlamini-Zuma dhidi ya mgombea anayetetea uenyekiti huo, Bw. Jean Ping.

Nchi Wanachama wa AU zinatarajiwa kupiga kura na hatimaye kumchagua Mwenyekiti wa Kamisheni hiyo mwezi wa Julai mwaka huu wakati wa Mkutano wa Wakuu wa Nchi mjini Lilongwe, nchini Malawi. 






Tuesday, May 8, 2012

Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (MB), atafanya mazungumzo na waandishi wa habari kwenye Ukumbi wa Mikutano Wizarani tarehe 09 Mei, 2012 kuanzia saa tano asubuhi.

Masuala atakayozungumzia ni pamoja na kampeni za mgombea wa nafasi ya Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika (AU), Bi. Nkosazana Dlamini-Zuma, anayeungwa mkono na Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC).

Imetolewa na,

KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI,
WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA,
DAR ES SALAAM.

08 MEI, 2012

Sunday, April 29, 2012

Wakuu wa Nchi wa EAC wasaini Itifaki ya Mkataba wa masuala ya Ulinzi



Mhe. Rais Jakaya Mrisho Kikwete (wa pili kushoto), akiwa na viongozi wenzake wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wakitia saini Mkataba wa makubaliano ya ushirikiano katika ulinzi.  Sherehe hiyo ilifanyika Ngurdoto Lodge tarehe 28 Aprili, 2012.  (picha na Ikulu)

Na ROSEMARY MALALE, Arusha
28 Aprili, 2012
Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wameridhia na kusaini Itifaki ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Ushirikiano katika masuala ya Ulinzi na kuelekeza kuanza mara moja kwa  majadiliano ya pamoja yatakayopelekea kukamilika kwa Mkataba wa Pamoja katika masuala ya Ulinzi.
Aidha, mbali na kutia saini Itifaki hiyo Wakuu hao wa Nchi waliipokea ripoti iliyowasilishwa kwao na Baraza la Mawaziri na kuridhia masuala mbalimbali katika ripoti hiyo ikiwa ni pamoja na kumteua Bi. Jesca Eriyo, kutoka Uganda kuwa Naibu Katibu Mkuu mpya  kufuatia aliyekuwepo Bibi Beartice Kiraso kumaliza muda wake wa kazi katika Jumuiya.
Vilevile Wakuu wa Nchi wa Jumuiya hiyo waliridhia pendekezo la kumuongezea mkataba wa miaka  mingine mitatu  Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo Bw. Jean Clausde Nsengiyumva kutoka Burundi.
Kuhusu maombi ya Sudan Kusini ya kuwa Mwanachama wa Jumuiya hiyo, wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wamekubali mapendekezo ya Baraza la Mawaziri ya kuundwa kwa Timu ya Uhakiki itakayohusisha wataalam watatu kutoka kila nchi mwanachama na Wataalam watatu kutoka katika Sekretarieti ya Jumuiya hiyo kwa ajili ya kuwezesha zoezi hilo.
Timu hiyo ya uhakiki, pamoja na mambo mengine itapitia maombi ya nchi hiyo na kuona kama yanakidhi Vigezo vya Mkataba ulioanzisha Jumuiya ya Afrika Mashariki ili kuwa mwanachama. Vigezo hivyo ni pamoja na masuala ya kijiografia yaani kama nchi ya Sudan Kusini inapakana au ipo karibu na mojawapo ya nchi mwanachama wa jumuiya hiyo;   nchi kuzingatia kanuni na misingi ya kimataifa ya demokrasia, utawala wa sheria, kuheshimu haki za binadamu, utawala bora na mchango wan chi katika kuimarisha ushirikiano ndani ya Jumuiya.
Wakuu hao wan chi pia walizungumzia masuala ya usalama katika kanda ya Afrika Mashariki ikiwa ni pamoja na mgogoro unaoendelea baina ya Sudan na Sudan Kusini na kuzitaka nchi hizo kurudi kwenye meza ya mazungumzo kumaliza tofauti zao.
Awali akifungua mkutano huo, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Tanzania na mwenyeji wa mkutano aliwakaribisha nchini marais na viongozi mbalimbali kutoka nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na kueleza kuwa ni imani yake kuwa mkutano huo utakuwa ni wa mafanikio makubwa kwa manufaa ya wananchi wa Afrika Mashariki kwa ujumla.
“Sitapenda kuchukua muda mwingi kuzungumza siku ya leo bali nawakaribisha sana Tanzania na hasa hapa Arusha na ni imani yangu kuwa mkutano huu utakuwa wa mafanikio na manufaa kwa wananchi wa Jumuiya hii,” alisema Mhe. Kikwete.
Aidha, katika hotuba yake Mhe. Mwai Kibaki, Rais wa Kenya  ambaye pia ni Mwenyekiti wa sasa wa Jumuiya hiyo alieleza kuwa kuna umuhimu kwa nchi wanachama kuimarisha na kuwa na mtandao wa pamoja  wa miundombinu ili kukuza biashara na uchumi kwa ujumla.
Mkutano huo Maalum wa 10 wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ulifanyika mjini Arusha tarehe 28 Aprili, 2012 na kuhudhuriwa na Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Tanzania, Mhe. Yoweri Kaguta Museveni, Rais wa Uganda, Mhe. Mwai Kibaki, Rais wa Kenya na Mhe. Paul Kagame, Rais wa Rwanda.
Wengine ni Mhe. Therence Sinunguruza Makamu wa Kwanza wa Rais wa Burundi, Mhe. Balozi Seif Ali Iddi, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mawaziri, Makatibu Wakuu, Mabalozi na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa hapa nchini na wadau mbalimbali.

-Mwisho-

Saturday, April 28, 2012

World Leaders congratulate President Kikwete


Leaders from different parts of the world have continued to congratulate H.E. Dr. Jakaya Mrisho Kikwete, the President of the United Republic of Tanzania upon marking 48th Anniversary of the Union between Tanganyika and Zanzibar on April 26, 2012.

H.E. Kim Yong Nam, the President of the Presidium of the Supreme People’s Assembly of the Democratic People’s Republic of Korea said the government and people of Tanzania have achieved a greater success in the work for national unity and economic development.

"I take this opportunity to wish you greater success in your and your people’s efforts for development and prosperity of the country,” he said.

On his part, the President of the French Republic, Mr. Nicolas Sarkozy said his country shares the international commitment of Tanzania in favor of democracy, good governance and development, and appreciates Tanzania contribution to the peace and strengthening regional integration in Africa.

"I am delighted about the presence of the United Republic of Tanzania in the Peace and Security Council of the African Union, and tanzania's readness in furthering dialogue on regional security issues between our two countries.”

The President of the Republic of Turkey, H.E. Abdullah GÏ‹l, told the Tanzanian President that his country cherishes the achievement attained so far saying he was confident that Tanzania will remain determined to stay the course for development and enhancing bilateral ties between the two countries.”

H.E. Mr. Truong Tan Sang, the President of Vietnam said Tanzanians under the able leadership of President Kikwete have managed to attain a tremendous achievements while maintaining peace and unity of its people.

President of the Islamic Republic of Pakistan, H.E. Mr. Asif Ali Zardari, said Pakistan and Tanzania have historically maintained and nurtured very close, cordial and cooperation relations in diverse fields and called for a sustained and continued progress of the people and economic development of Tanzania.

President Kikwete also received the goodwill messages from Sultan of Oman, the Republic of Benin, Mexico and Hellenic Republic of Greece.

Issued by:

THE MINISTRY OF FOREIGN AFFAIRS AND INTERNATIONAL COOPERATION,

DAR ES SALAAM

APRIL 28, 2012

Friday, April 27, 2012

Rais Kibaki ahudhuria Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa EAC




Rais wa Kenya, Mhe. Mwai Kibaki, akipokelewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (MB), mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) mjini Arusha jana.  Rais Kibaki anahudhuria Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki unaofanyika leo tarehe 28 Aprili 2012.



Rais Kibaki wa Kenya, akitumbuizwa na burudani ya ngoma mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) jana mjini Arusha.


Rais Kibaki wa Kenya (katikati), akiwa na wenyeji wake Mhe. Membe (kulia) na Mhe. Samuel Sitta (kushoto), Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, mara baada ya kuwasili jana mjini Arusha.



Thursday, April 26, 2012

MKUTANO WA BARAZA LA MAWAZIRI WA EAC


Mhe. Bernard K. Membe (Mb.), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa (wa katikati mstari wa mbele) akiwa na Mhe. Hussein Mwinyi (Mb.), Waziri wa Ulinzi pamoja na Mhe. Harrison Mwakyembe (Mb.), Naibu Waziri wa Ujenzi kwenye moja ya vikao vya majadiliano vya ujumbe wa Tanzania kabla ya Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika mjini Arusha tarehe 25 Aprili, 2012. (Picha na Wizara ya Mambo ya Nje).


Mabalozi wa Tanzania katika nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki wakiwa katika moja ya vikao vya majadiliano wakati wa Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya hiyo uliofanyika jana mjini Arusha. Kutoka kushoto ni Dkt. Batilda Buriani, Balozi wa Tanzania, Kenya, Mhe. Marwa Matiko, Balozi wa Tanzania, Rwanda, Mhe. James Nzagi, Balozi wa Tanzania, burundi na Mhe. Dkt. Ladislaus Komba, Balozi wa Tanzania, Uganda.


Mhe. Samwel Sitta, Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Kiongozi wa Ujumbe wa Tanzania kwenye mkutano wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki akiwa na Katibu Mkuu wa Wizara yake, Dkt. Stergomena Tax-Bamwenda akiongoza moja ya vikao vya majadiliano vya ujumbe wa Tanzania (haupo pichani) kabla ya Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya hiyo uliofanyika Arusha tarehe 25 Aprili, 2012.


Bw. John Haule, Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akibadilishana mawazo na Bw. George Masaju, Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali wakati wa Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki jana mjini Arusha.


Mhe. Samwel Sitta, Waziri wa Afrika Mashariki, akiwa na baadhi ya Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wakisaini Ripoti  baada ya kufikia makubaliano katika mkutano wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya hiyo uliofanyika jana mjini Arusha. 

26 Aprili, 2012
Na ROSEMARY MALALE, ARUSHA
Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki umefanyika mjini Arusha jana kujadili na kukubaliana agenda mbalimbali zitakazowasilishwa kwenye Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya hiyo tarehe 28 Aprili, 2012.

Miongoni mwa agenda muhimu zilizojadiliwa na Mawaziri hao ni pamoja na mapendekezo ya kuteua Naibu Katibu Mkuu  mpya kutoka Uganda kufuatia aliyekuwepo Bibi Beartice Kiraso kumaliza muda wake; kuongeza mkataba wa miaka mitatu kwa Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo Bw. Jean Claude Nsengiyumva kutoka Burundi; kupitia ripoti kuhusu maombi ya Jamhuri ya Sudan Kusini ya kuwa mwanachama wa Jumuiya na kupitia Mswada wa sheria ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kuhusu uangalizi wa uzito wa mizigo inayobebwa na magari ili kulinda barabara za nchi wanachama zisiharibiwe.
Masuala mengine yaliyojadiliwa ni Rasimu ya Itifaki ya Kupambana na Rushwa kwa nchi wanachama; Rasimu ya Itifaki ya Ushirikiano katika masuala ya Ulinzi na ripoti ya Kamati ya Fedha na Utawala.
Awali akifungua Mkutano huo wa Baraza la Mawaziri, Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo Dkt. Richard Sezibera aliwaomba Mawaziri watoe maoni yao kuhusu agenda hizo ili baadae zifikishwe na kuridhiwa na Wakuu wa Nchi.
Mkutano huo wa Mawaziri ulitanguliwa na vikao vya Maafisa Waandamizi kutoka nchi wanachama kilichofanyika tarehe 20-22 Aprili kikifuatiwa na kikao cha Kamati ya Uratibu chini ya Makatibu Wakuu kutoka nchi wanachama kilichofanyika tarehe 23 na 24 Aprili, 2012.
Ujumbe wa Tanzania kwenye mkutano huo  uliongozwa na Mhe. Samwel Sitta (Mb), Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki na kuwahusisha pia Mhe. Bernard K. Membe (Mb), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Hussein Mwinyi (Mb), Waziri wa Ulinzi, Mhe. Perreira Ame Silima (Mb), Naibu Waziri wa Fedha na Mhe. Harrison Mwakyembe (Mb), Naibu Waziri wa Ujenzi.
Wengine ni Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Bw. George Masaju, Dkt. Stergomena Tax-Bamwenda, Katibu Mkuu wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. John Haule, Katibu Mkuu wa Mambo ya  Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Herbert Mrango, Katibu Mkuu wa Ujenzi, Bw. Job Masima, Katibu Mkuu wa Ulinzi, Mabalozi wa Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi na Maafisa Waandamizi  kutoka Serikalini.
Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki utafanyika mjini hapa tarehe 28 Aprili, 2012.